Maelezo ya Chini
c Asili ya jina hilo imezua ubishi miongoni mwa wasomi. Katika Kiebrania, jina Musa linamaanisha “Kuchotwa; Kuokolewa Kutoka Majini.” Mwanahistoria Flavius Josephus alisema kwamba jina Musa limeundwa kwa maneno mawili ya Kimisri yanayomaanisha “maji” na “kuokolewa.” Leo vilevile, wasomi fulani wanaamini kwamba jina Musa ni la asili ya Kimisri lakini wanaona kwamba huenda linamaanisha “Mwana.” Hiyo ni kwa sababu neno “Musa” linatamkwa sawa na majina fulani ya Kimisri. Kwa kuwa hakuna anayejua jinsi Kiebrania au Kimisri cha kale kilivyotamkwa, dhana hizo ni za kukisia tu.