Maelezo ya Chini
d Kitabu Israel in Egypt kinasema: “Dhana ya kwamba Musa alilelewa katika jumba la kifalme la Misri inaonekana kuwa hadithi tu. Lakini uchunguzi wa makini wa jumba la kifalme wakati wa falme za kati ya mwaka wa 1550 mpaka 1070 K.W.K. hivi, hauungi mkono dhana hiyo. Mfalme Thutmose wa 3 . . . alianzisha zoea la kuwapeleka Misri wana wa wafalme vibaraka wa mataifa ya magharibi mwa Asia ili wazoezwe desturi za Misri . . . Hivyo, wana na binti za wafalme wa mataifa mengine walikuwapo katika jumba la kifalme la Misri.”