Maelezo ya Chini
f Katika majaribio mengi ya kubadili chembe za urithi, idadi ya viumbe wapya ilizidi kupungua huku aina zilezile za mimea na wanyama zikitokezwa. Hilo lilimfanya Lönnig aanzishe “sheria ya mabadiliko yanayojirudia-rudia.” Isitoshe, chini ya asilimia 1 ya mimea iliyotokezwa kwa kubadili chembe za urithi ilitumiwa katika uchunguzi zaidi, na chini ya asilimia 1 ya mimea hiyo ndiyo ilifaa kwa matumizi ya kibiashara. Matokeo ya utafiti uliohusisha wanyama yalikuwa mabaya sana kuliko yale ya mimea hivi kwamba majaribio hayo yakasimamishwa.