Maelezo ya Chini
c Wenzi wa ndoa ambao ni Mashahidi wa Yehova wanaweza kuwasiliana na Halmashauri ya Uhusiano na Hospitali (HLC) ya Mashahidi wa Yehova katika eneo lao kabla ya kujifungua. Washiriki wa halmashauri hiyo hutembelea hospitali na madaktari ili kuwapa habari kuhusu matibabu yasiyohusisha damu ambayo wagonjwa Mashahidi hukubali. Isitoshe, halmashauri hizo zinaweza kusaidia kumpata daktari anayeheshimu imani ya wagonjwa na aliye na uzoefu wa kutibu wagonjwa bila damu.