Maelezo ya Chini
a Inaonekana kwamba wazo hilo lilitokana na maandishi ya askofu Mhispania, Isidore wa Seville (560-636 W.K.), aliyesema hivi: “Kuna lugha tatu takatifu, Kiebrania, Kigiriki, na Kilatini, na hizo ndizo lugha kuu ulimwenguni pote. Sababu ni kwamba shtaka dhidi ya Bwana lililoandikwa juu ya msalaba na Pilato lilikuwa katika lugha hizo tatu.” Bila shaka, uamuzi wa kuandika shtaka hilo katika lugha hizo tatu ulifanywa na Waroma wapagani. Uamuzi huo haukutoka kwa Mungu.