Maelezo ya Chini
a Watu fulani wanatoa sababu nyingine: Labda Wayahudi walivutwa na falsafa ya Kigiriki. Kwa mfano, Filo, mwanafalsafa wa Kiyahudi wa Aleksandria ambaye karibu aliishi wakati mmoja na Yesu, alivutwa sana na Plato, mwanafalsafa Mgiriki, aliyefikiriwa na yeye kuwa aliongozwa na roho ya Mungu. Kichapo Lexicon des Judentums (Kamusi ya Mambo ya Wayahudi), kinaeleza chini ya “Philo,” kwamba Filo ‘aliunganisha lugha na mawazo ya falsafa ya Kigiriki (Plato) pamoja na imani ya Wayahudi iliyofunuliwa’ na ya kwamba jambo la kwanza yeye ‘alikuwa na uvutano wa waziwazi juu ya mababa wa kanisa la Kikristo.’ Filo alifundisha kwamba Mungu alikuwa asiyeelezeka na, kwa sababu hiyo, asiye na jina.