Maelezo ya Chini
b Mazungumzo yenye habari nyingi juu ya namna viongozi wa kidini walivyounga mkono Vita ya Ulimwengu ya Kwanza yanatolewa katika kitabu Preachers Present Arms, cha Ray H. Abrams (New York, 1933). Kitabu hicho kinasema hivi: “Viongozi wa kidini walivipa vita umaana wa juhudi yao ya kiroho na msukumo. . . . Vita yenyewe ilikuwa ni vita takatifu ya kuendeleza Ufalme wa Mungu duniani. Mtu kutoa uhai wake kwa ajili ya nchi yake kulikuwa ni kuutoa kwa ajili ya Mungu na Ufalme Wake. Mungu na nchi yakaja kuwa maneno yenye maana moja. . . . Wajeremani na Marafiki walikuwa sawa katika jambo hilo. Kila upande uliamini kwamba Mungu alikuwa upande wao . . . Wengi wa walimu wa kidini hawakuona ugumu wo wote katika kumweka Yesu katika mstari wa mbele kabisa panapopiganiwa vita vikali akiongoza vikosi vyao kwenye ushindi. . . . Kwa njia hiyo kanisa likaja kuwa sehemu ya mfumo wa vita. . . . Viongozi [wa makanisa] hawakupoteza wakati wo wote wakijitayarisha wakati wa vita. Kwa muda wa saa ishirini na nne tu baada ya kutangazwa vita, Baraza la Muungano wa Makanisa ya Kristo Katika Amerika lilifanya mpango wa kutoa ushirikiano kamili. . . . Makanisa mengi yalifanya mengi zaidi ya yale yaliyoombwa yafanye. Yakawa vituo vya kuandikisha askari wapya kwa ajili ya vikosi.”—Kurasa 53, 57, 59, 63, 74, 80, 82.