Maelezo ya Chini
c Mafundisho ya Dini ya Buddha, kama vile anatta (hakuna hatinafsi), hukanusha maisha yasiyobadilika au nafsi ya milele. Hata hivyo, wafuasi wa Dini ya Buddha walio wengi leo, hasa wale katika Mashariki ya Mbali, huamini kuhama kwa nafsi isiyoweza kufa kuingia katika mwili mwingine. Zoea lao la kuabudu wazazi wa kale waliokufa na imani katika helo baada ya kifo hudhihirisha hili.