Maelezo ya Chini
k George Howard, profesa-mshirika wa dini na Kiebrania kwenye Chuo Kikuu cha Georgia, atoa taarifa hii: “Kwa kadiri wakati ulivyopita, watu hao wawili [Mungu na Kristo] waliletwa kwenye umoja wa karibu hata zaidi hivi kwamba mara nyingi ikawa haiwezekani kutofautisha kati yao. Kwa hiyo yaweza kuwa kwamba kuondolewa kwa Tetragrammatoni kulichangia sehemu kubwa ya mabishano juu ya Kristo na Utatu yaliyotatiza kanisa la karne za mapema. Vyovyote iwavyo, kuondolewa kwa Tetragrammatoni yawezekana kulitokeza mazingira ya kitheolojia yaliyo tofauti na yale yaliyokuwapo wakati wa muhula wa Agano Jipya wa karne ya kwanza.”—Biblical Archaeology Review, Machi 1978.