Maelezo ya Chini
b Lutheri alisisitiza mno wazo la “kuhesabiwa haki kwa imani pekee” hivi kwamba katika tafsiri yake ya Biblia, aliongeza neno “pekee” kwa Warumi 3:28. Pia yeye alitilia shaka kitabu cha Yakobo kwa ajili ya taarifa ya kwamba “imani isipokuwa na matendo, imekufa.” (Yakobo 2:17, 26) Yeye alishindwa kutambua kwamba katika Warumi, Paulo alikuwa akinena juu ya matendo ya Sheria ya Kiyahudi.—Warumi 3:19, 20, 28.