Maelezo ya Chini
c Kigezo cha kisheria kilichotiwa na Musa katika fungu la sheria kwa kurejezea namna ya malipo kwa ajili ya uhalifu mbalimbali wa Sheria—“uhai kwa uhai, jicho kwa jicho, jino kwa jino”—huonyesha kanuni yenye kuongoza iliyotumiwa na Mungu mwenyewe katika kutatua suala la wokovu wa binadamu. (Kumbukumbu la Torati 19:21) Mwanadamu mkamilifu, Adamu, alikuwa amekuwa mwenye kulaumika kwa ajili ya hukumu ya laana ya jamii ya kibinadamu, hivyo mwanamume mwingine mkamilifu alihitajiwa ili kulipia dhambi ya Adamu na matokeo yayo kwa ainabinadamu. Ni kuja tu kwa “mbegu” aliyeahidiwa, ambaye uhai wake ungetolewa kuwa fidia ya kisheria, ndiye angeweza kutimiza kufunguliwa huko. (Mwanzo 3:15, JP) Kwa mazungumzo kamili zaidi ya upande huo wa Mbegu katika kusudi la Mungu, ona sehemu “Ni Nani Ataongoza Mataifa Kwenye Amani?,” mafungu 17 hadi 20.