Maelezo ya Chini
d Ufafanuzi uliokubaliwa wa Dini ya Kiyahudi ya ki-siku-hizi ni kwamba Yeremia alikuwa akitabiri tu kufanywa upya na kuthibitishwa upya kwa agano la Sheria pamoja na Israeli, kama ilivyotukia baada ya kurudi kwao kutoka uhamisho katika Babuloni katika 537 K.W.K. (Ezra 10:1-14) Lakini kwa mara nyingine tena unabii wenyewe hukanusha ufafanuzi kama huo. Mungu alitaarifu waziwazi kwamba hilo litakuwa “agano jipya,” si agano lililofanywa upya tu. Zaidi ya hilo, yeye akazia kwamba si kama lile agano lililofanywa wakati alipowaongoza kutoka katika utumwa wa Misri. Baadhi yao wamesema kwamba lilikuwa “jipya” katika maana ya kwamba sasa wangelishika kwa uaminifu agano lilo hilo, lakini historia huonyesha tofauti. Kwa kweli, ukosefu wao wa uaminifu uliongoza kwenye uharibifu wa lile hekalu la pili.—Kumbukumbu la Torati 18:19; 28:45-48.