Maelezo ya Chini
c Katika Kiebrania cha Biblia neno linalotafsiriwa “nafsi” ni neʹphesh. Hata hivyo, katika Dini ya Kiyahudi ya leo, neno la Kiebrania nesha·mahʹ mara nyingi hufikiriwa kuwa sehemu ya mwanadamu ambayo huendelea kuishi baada ya kifo. Lakini funzo la uangalifu la Maandiko hufunua kwamba neno nesha·mahʹ halikuwasilisha kamwe maana kama hiyo; hilo hurejezea tu ile njia ya kupumua au kiumbe chenye kupumua, binadamu au mnyama.—Mwanzo 7:22; Kumbukumbu la Torati 20:16; Yoshua 10:39, 40; 11:11; Isaya 2:22.