Maelezo ya Chini
b Miongoni mwa Wayahudi wa karne ya kwanza, mlikuwamo uelewevu wa ujumla kwamba unabii huo ungetimia katika wakati wao wenyewe. (Luka 3:15) Katika kitabu chake De Termino Vitae (Kuhusu Mwisho wa Maisha), rabi mmoja wa karne ya 17, Menasseh ben Israel, aliandika hivi: “Wengine wangekubali hayo majuma 70 kuwa yamaanisha kwamba baada ya mwisho wayo Mesiya angekuja ambaye angewafanya kuwa watawala wa ulimwengu wote. Kweli kweli, wote waliochukua silaha dhidi ya Waroma wakati ule walikuwa na maoni hayo.”