Maelezo ya Chini
b Katika Septemba 1945, Ndugu Covington alikataa kwa moyo mzuri kutumikia zaidi akiwa makamu wa msimamizi wa Watch Tower Bible and Tract Society (ya Pennsylvania), akieleza kwamba alitaka kukubaliana na yaliyoeleweka wakati huo kuwa mapenzi ya Yehova kwa washiriki wote wa baraza la waelekezi na maofisa—kwamba wawe Wakristo waliotiwa mafuta kwa roho, hali yeye alidai kuwa mmoja wa “kondoo wengine.” Oktoba 1, Lyman A. Swingle alichaguliwa kwenye baraza la waelekezi, na Oktoba 5, Frederick W. Franz akachaguliwa kuwa makamu wa msimamizi. (Ona Kitabu-Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 1946, cha Kiingereza, kur. 221-224; Mnara wa Mlinzi, Novemba 1, 1945, kur. 335-336.)