Maelezo ya Chini
g Katika mazungumzo yenye habari nyingi zaidi juu ya jambo hili, katika 1955, kijitabu What Do the Scriptures Say About “Survival After Death”? kilionyesha kwamba maandishi ya Biblia huonyesha kwamba kwa kweli Shetani alimtia Hawa moyo aamini kwamba yeye hangekufa katika mwili kama matokeo ya kupuuza katazo la Mungu juu ya kula tunda kutoka kwa “mti wa ujuzi wa mema na mabaya.” (Mwa. 2:16, 17; 3:4) Baada ya wakati, kwa wazi hilo lilithibitika kuwa si kweli, lakini kulikuwa na matukio zaidi yaliyokuwa na shina katika uwongo huo wa kwanza. Watu walikubali maoni ya kwamba sehemu isiyoonekana ya mtu huendelea kuishi. Kufuatia Furiko la siku ya Nuhu, hilo liliimarishwa na mazoea ya kimashetani ya roho waovu yaliyokuwa yakitoka Babiloni.—Isa. 47:1, 12; Kum. 18:10, 11.