Maelezo ya Chini
i Hilo liliongozwa na imani ya kwamba mileani ya saba ya historia ya kibinadamu ilikuwa imeanza katika 1873 na kwamba kipindi cha kutokuwa na upendeleo wa kimungu (cha urefu sawa na kipindi kilichotangulia kilichofikiriwa kuwa cha upendeleo) juu ya Israeli wa asili kingekoma katika 1878. Kronolojia hiyo ilikuwa na kosa kwa sababu ya kutegemea tafsiri isiyo sahihi ya Matendo 13:20 katika King James Version, imani ya kwamba kulikuwa kosa la kunakili kwenye 1 Wafalme 6:1, na kushindwa kufikiria kronolojia ya Kibiblia katika kuweka tarehe za milki za wafalme wa Yuda na wa Israeli. Uelewevu ulio wazi zaidi wa kronolojia ya Biblia ulitangazwa katika 1943, katika kitabu “The Truth Shall Make You Free,” halafu ukafanywa kuwa bora mwaka uliofuata katika kitabu “The Kingdom Is at Hand,” na pia katika vichapo vya baadaye.