Maelezo ya Chini
c Nyakati nyingine vikundi vya mahali vilirejezewa kuwa “makanisa,” kupatana na lugha inayotumiwa katika Biblia ya Kiswahili. Yaliitwa pia eklesia, kupatana na neno linalotumiwa katika maandishi ya Biblia ya Kigiriki. Neno “madarasa” vilevile lilitumiwa, maana kwa kweli walikuwa vikundi vya wanafunzi waliokutana kwa ukawaida kwa ajili ya funzo. Baadaye, walipoitwa kampuni, hilo lilionyesha kujua kwao kwamba walikuwa katika vita ya kiroho. (Ona Zaburi 68:11, KJ, pambizoni.) Baada ya kutangazwa kwa New World Translation of the Christian Greek Scriptures katika 1950, neno “kutaniko” la lugha ya Biblia ya kisasa likaja kutumiwa kwa ukawaida katika nchi nyingi zaidi.