Maelezo ya Chini
b Maneno hayo yalitegemea uelewevu kwamba neno dini lilitia ndani ibada yote inayotegemea mapokeo ya wanadamu, badala ya kutegemea Neno la Mungu, Biblia. Hata hivyo, katika 1950, wakati Biblia New World Translation of the Christian Greek Scriptures ilipotangazwa, vielezi-chini kwenye Matendo 26:5, Wakolosai 2:18, na Yakobo 1:26, 27 vilionyesha kwamba neno dini lingeweza kutumiwa kwa kufaa kuelekeza kwa ibada ya kweli au ya bandia. Hilo lilieleweshwa zaidi katika Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) la Machi 15, 1951, ukurasa 191, na kitabu What Has Religion Done for Mankind?, kurasa 8-10.