Maelezo ya Chini
d Hakimu wa Mzunguko Martin T. Manton, wa Katoliki ya Roma aliye mshupavu, alikataa rufani ya pili ya kupewa dhamana Julai 1, 1918. Wakati mahakama ya kitaifa ya rufani ilipobatilisha hukumu ya washtakiwa, Manton pekee ndiye ambaye hakupendelea hilo. Inastahili kuangaliwa kwamba Desemba 4, 1939, mahakama ya rufani iliyofanyizwa kipekee ilitetea kuhukumiwa kwa Manton kwa ajili ya utumizi mbaya wa uwezo wa mahakama, kutokuwa mnyoofu, na kutumia hila.