Maelezo ya Chini
e Jambo la kwamba wanaume hao walifungwa isivyo haki, na hawakuwa wenye hatia, linaonyeshwa na uhakika wa kwamba J. F. Rutherford aliendelea kuwa mshiriki wa mawakili wa Mahakama Kuu ya Marekani tangu kusajiliwa kwake katika Mei 1909 hadi kifo chake katika 1942. Katika kesi 14 zilizokatwa rufani katika Mahakama Kuu kuanzia 1939 hadi 1942, J. F. Rutherford alikuwa mmoja wa mawakili. Katika kesi zilizoitwa Schneider v. State of New Jersey (katika 1939) na Minersville School District v. Gobitis (katika 1940), yeye mwenyewe alitoa hoja za maneno mbele ya Mahakama Kuu. Pia, wakati wa Vita ya Ulimwengu 2, A. H. Macmillan, mmojawapo wanaume waliofungwa isivyo haki mwaka 1918-1919, alikubaliwa na mkurugenzi wa Idara ya Magereza ya kitaifa kuwa akifanya ziara za kawaida kwenye magereza ya kitaifa ya Marekani ili kutunza faida za kiroho za vijana waliokuwa huko kwa sababu ya kuwa wamechukua msimamo wa kutokuwamo kwa Kikristo.