Maelezo ya Chini
b Ukiwa mwongozo wa ujumla, walipopelekwa mahakamani kwa sababu ya kutoa ushahidi, Mashahidi wa Yehova walikata rufani ya kesi zao badala ya kulipa faini. Ikiwa walishindwa kesi baada ya rufani kusikizwa, basi badala ya kulipa faini, walienda gerezani, iwapo waliruhusiwa kufanya hivyo na sheria. Kukataakataa kwa Mashahidi kulipa faini kulisaidia kuvunja moyo maofisa fulani wasiendelee kuingilia utendaji wao wa kutoa ushahidi. Ingawa mwongozo huo ungali waweza kufuatwa katika hali fulani, Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) la Aprili 1, 1975, lilionyesha kwamba katika visa vingi faini ingeweza kuonwa kwa kufaa kuwa adhabu ya kisheria, kwa hiyo kuilipa hakungekuwa ni kukubali hatia, kama vile kwenda gerezani hakungemthibitisha mtu kuwa mwenye hatia.