Maelezo ya Chini
b Ni kweli kwamba tafsiri ya Septuagint ya Kigiriki ilikuwa msingi wa manukuu ya Maandiko ya Kiebrania katika lile lenye kuitwa isivyofaa, Agano Jipya. Kwa kuwa nakala za baadaye za Septuagint hazina jina la kimungu, wasomi wengi hujadili kwamba jina hilo halipaswi vilevile kutiwa ndani katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Hata hivyo, nakala zilizoko za zamani zaidi za Septuagint zina hilo jina Yehova—katika namna yalo ya Kiebrania cha awali. Hilo lategemeza kwa nguvu kule kurudishwa kwa jina Yehova katika Maandiko ya Kigiriki.