Maelezo ya Chini
a Biblia fulani-fulani hutumia neno “ulimwengu” badala ya “mfumo wa mambo.” Kamusi iitwayo Expository Dictionary of New Testament Words ya W. E. Vine, husema kwamba neno la Kigiriki ai·onʹ “humaanisha kipindi cha muda usio dhahiri, au wakati unaoonwa kwa kuhusiana na yale yanayotukia katika hicho kipindi.” Nayo kamusi iitwayo Greek and English Lexicon to the New Testament ya Parkhurst (ukurasa 17) hutia ndani usemi “mfumo huu wa mambo” katika kuzungumzia matumizi ya ai·oʹnes (kwa wingi) kwenye Waebrania 1:2. Kwa hiyo fasiri hii “mfumo wa mambo” inapatana na maandishi-awali ya awali ya Kigiriki.