Maelezo ya Chini
e Mwaka wa 1900, urefu wa uhai katika nchi nyingi za Ulaya na katika Marekani ulitarajiwa kuwa usiozidi miaka 50. Tangu wakati huo, urefu huo umeongezeka kwa njia ya kutazamisha si kwa sababu tu ya maendeleo ya kitiba katika kudhibiti maradhi bali pia kwa sababu ya usafi wa kutunza afya na hali nzuri zaidi za maisha.