Maelezo ya Chini
b Mwanzo 2:17 lataja amri ya Mungu kwa Adamu asile kutokana na mti wa ujuzi wa wema na uovu. Katika kielezi-chini cha andiko hilo, The New Jerusalem Bible (1985) inasema hivi kuhusu kilichomaanishwa na ujuzi huo: “Ni uwezo wa kujiamulia lililo jema na lililo ovu na kutenda kwa kupatana na uamuzi huo, dai la kuwa huru kabisa kimaadili ambalo katika hilo mwanadamu anakataa kutambua kwamba yeye ni kiumbe kilichoumbwa, ona Is[aya] 5:20. Dhambi ya kwanza ilikuwa kushambulia enzi kuu ya Mungu.”