Maelezo ya Chini
a Wachambuzi fulani hujaribu kupunguza lile shtaka la udanganyifu kwa kusema kwamba mwandikaji alitumia jina Danieli likiwa jina bandia, kama vile vichapo vya kale visivyo vya maandiko yaliyokubalika vilivyoandikwa kwa kutumia majina bandia. Hata hivyo, mchambuzi wa Biblia Ferdinand Hitzig alisisitiza hivi: “Kusema kwamba kitabu cha Danieli kiliandikwa na [mwandikaji] mwingine, si sawa na kutumia jina bandia. Kusema hivyo kwakifanya kiwe maandishi ya udanganyifu, na lengo lilikuwa kudanganya wasomaji wake, ingawa ni kwa manufaa yao.”