Maelezo ya Chini
a Kwa mujibu wa mapokeo ya kale ya Wayahudi, Mfalme Manase mwovu alifanya Isaya auawe, akatwe vipande-vipande kwa msumeno. (Linganisha Waebrania 11:37.) Chanzo kimoja chasema kuwa nabii fulani asiye wa kweli alileta mashtaka yafuatayo juu ya Isaya, ili apewe adhabu hiyo ya kifo: “Ameliita Yerusalemu Sodoma, naye amewatangaza wakuu wa Yuda na Yerusalemu (kuwa) watu wa Gomora.”