Maelezo ya Chini
a Wasomi fulani hudokeza kuwa usemi ‘chipukizi la Yehova’ humrejezea kwa njia isiyo ya moja kwa moja, Mesiya ambaye hangetokea kabla ya kurudishwa kwa Yerusalemu. Katika Targum za Kiaramu, fungu hilo lasimuliwa hivi kwa maneno mengine: “Mesiya [Kristo] wa Yehova.” Kwa kupendeza, baadaye Yeremia alitumia neno hilohilo la Kiebrania (tseʹmach) anapozungumza juu ya Mesiya akiwa kama “chipukizi la haki” analochipushiwa Daudi.—Yeremia 23:5; 33:15.