Maelezo ya Chini
a Isaya 9:8–10:4 ina beti nne (mafungu ya shairi), kila mmoja ukimalizika kwa kibwagizo chenye kutisha: “Pamoja na hayo yote hasira yake haikugeukia mbali, lakini mkono wake umenyoshwa hata sasa.” (Isaya 9:12, 17, 21; 10:4) Mtindo huo wa kifasihi huunganisha Isaya 9:8–10:4 kuwa “neno” moja kuu. (Isaya 9:8) Pia ona kwamba “mkono [wa Yehova] umenyoshwa hata sasa,” si kwa ajili ya kuleta upatanisho, bali kuhukumu.—Isaya 9:13.