Maelezo ya Chini
b Waelezaji wengi wa Biblia hufikiri kuwa maneno “itieni ngao mafuta” yarejezea zoea la zamani la kijeshi la kutia mafuta kwenye ngao zao za ngozi kabla ya vita ndipo silaha nyingi zinazorushwa ziteleze. Ingawa fasiri hiyo huenda ikawa kweli, yapasa ikumbukwe kuwa usiku ambao jiji hilo lilianguka, Wababiloni hawakuwa na wakati wa kupigana, sembuse wa kujitayarishia vita kwa kutia ngao zao mafuta!