Maelezo ya Chini
b Baada ya kushindwa kwa Senakeribu, mataifa jirani yalimletea Hezekia zawadi za dhahabu, fedha, na vitu vingine vyenye thamani. Twasoma kwenye 2 Mambo ya Nyakati 32:22, 23, 27 kwamba “Hezekia akawa na mali nyingi mno na heshima” na kwamba “hata yeye akatukuka tangu wakati ule machoni pa mataifa yote.” Huenda zawadi hizo zilimwezesha kujaza tena nyumba yake ya hazina, ambayo alikuwa ameiacha tupu alipowalipa Waashuri ushuru.