Maelezo ya Chini
a Isaya atabiri kutengenezwa kwa njia mbele za Yehova. (Isaya 40:3) Hata hivyo, Gospeli zahusisha unabii huo na yale ambayo Yohana Mbatizaji alifanya kumtayarishia Yesu Kristo njia. Waandikaji waliopuliziwa wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo walifanya uhusiano huo kwa sababu Yesu alimwakilisha Baba yake naye alikuja katika jina la Baba yake.—Yohana 5:43; 8:29.