Maelezo ya Chini
a “Hakuna shaka kwamba Shetani alitambua kuwa Yesu ndiye Mwana wa Mungu na kwamba ndiye aliyetajwa na unabii kuwa atamponda kichwa (Mwa 3:15), na kwa hiyo alijaribu juu chini kumwangamiza Yesu. Lakini, malaika Gabrieli alipokuwa akimtangazia Maria kuhusu kutungwa mimba ya uhai wa Yesu, alimwambia hivi: ‘Roho takatifu itakuja juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Zaidi Sana itakufunika kivuli. Kwa sababu hiyo pia kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.’ (Lu 1:35) Yehova alimlinda Mwana wake. Jitihada za kumwangamiza Yesu akiwa kitoto kichanga hazikufaulu.”—Insight on the Scriptures, Buku la 2, ukurasa wa 868, lililochapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.