Maelezo ya Chini
c Neno la Kiebrania lililotafsiriwa ‘kupigwa kwa tauni’ linatumiwa pia kuhusu ukoma. (2 Wafalme 15:5) Wasomi fulani wanasema kwamba, wazo ambalo Wayahudi fulani walipata kutokana na Isaya 53:4 ni kwamba Mesiya angekuwa mwenye ukoma. Talmudi ya Kibabiloni hutumia mstari huu kuhusu Mesiya, ikimwita “yule msomi mwenye ukoma.” Tafsiri ya Kikatoliki iitwayo Douay Version, inatoa wazo moja na Vulgate ya Kilatini kwa kuufasiri mstari huo hivi: “Tumemfikiria kana kwamba ni mwenye ukoma.”