Maelezo ya Chini
d Mtume Yohana anatumia usemi kama huo anapoeleza kuhusu “Yerusalemu jipya,” wale 144,000 wakiwa katika utukufu wa kimbingu. (Ufunuo 3:12; 21:10, 22-26) Hiyo inafaa, kwa maana “Yerusalemu jipya” linawakilisha washirika wote wa Israeli wa Mungu baada ya wao kupokea thawabu yao ya kimbingu, na hivyo kujumlika pamoja na Yesu Kristo kuwa sehemu ya jiji kuu la “mwanamke” wa Mungu, “Yerusalemu la juu.”—Wagalatia 4:26.