Maelezo ya Chini
c Mafarisayo waliamini kwamba watu wa hali ya chini, ambao hawakujua Sheria, walikuwa watu “waliolaaniwa.” (Yohana 7:49) Walisema kwamba mtu hakupaswa kuwafundisha watu hao wala kufanya biashara nao wala kula nao wala kusali nao. Walisema kwamba mtu akimruhusu binti yake aolewe na mmoja wao lingekuwa jambo baya kuliko kumpeleka kwa wanyama wakali sana. Waliamini kwamba watu hao wa hali ya chini hawatafufuliwa.