Maelezo ya Chini
b Kwenye 2 Timotheo 4:2, Biblia inasema kwamba nyakati nyingine ni lazima wazee ‘wakaripie, wakemee, na kuhimiza kwa bidii.’ Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “himiza kwa bidii” (pa·ra·ka·leʹo) linaweza kumaanisha “kutia moyo.” Neno jingine la Kigiriki linalohusiana nalo, pa·raʹkle·tos, linaweza kumaanisha wakili wa kisheria. Kwa hiyo, hata wakati wazee wanapokaripia kwa uthabiti, wanapaswa kuwa wasaidizi wa wale wanaohitaji msaada wa kiroho.