Maelezo ya Chini
b Hati fulani za kale hazina sehemu ya kwanza ya Luka 23:34. Hata hivyo, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya na tafsiri nyingine nyingi zina maneno hayo kwa sababu yanapatikana kwenye hati nyingi mashuhuri. Ni wazi kwamba Yesu alikuwa akizungumza kuhusu askari Waroma ambao walimtundika mtini. Hawakujua walilokuwa wanafanya, kwa sababu hawakujua Yesu ni nani. Bila shaka, viongozi wa kidini ambao walichochea mauaji hayo walikuwa na hatia kubwa zaidi, kwa sababu walifanya hivyo kimakusudi na kwa nia mbaya. Wengi wao hawangeweza kusamehewa.—Yohana 11:45-53.