Maelezo ya Chini
e Kuharibiwa kwa Babiloni ni mfano mmoja tu wa unabii wa Biblia ambao umetimizwa. Mifano mingine inatia ndani kuharibiwa kwa Tiro na Ninawi. (Ezekieli 26:1-5; Sefania 2:13-15) Pia, unabii wa Danieli ulitabiri milki za ulimwengu ambazo zingetawala baada ya Babiloni. Zilitia ndani Ugiriki na muungano wa Umedi na Uajemi. (Danieli 8:5-7, 20-22) Unaweza kupata habari zaidi kuhusu unabii mbalimbali unaomhusu Masihi uliotimizwa na Yesu Kristo katika nyongeza “Yesu Kristo—Masihi Aliyeahidiwa.”