Maelezo ya Chini
a Yesu hakumwambia kila mtu aliyemfuata aache mali zake zote. Na ingawa alisema ingekuwa vigumu sana kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu, aliongeza hivi: “Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.” (Marko 10:23, 27) Kwa kweli, baadhi ya wafuasi wa Kristo walikuwa matajiri. Walipata mashauri hususa katika kutaniko la Kikristo, lakini hawakuagizwa wawape maskini mali zao zote.—1 Timotheo 6:17.