Maelezo ya Chini
b Biblia inaonyesha kwamba mtu hapaswi kutosheka kwa sababu tu dhamiri yake haimsumbui. Kwa mfano, Paulo alisema: “Sifahamu kitu chochote dhidi yangu mwenyewe. Lakini kwa hilo sionyeshwi kuwa mwadilifu, bali yeye anayenichunguza ni Yehova.” (1 Wakorintho 4:4) Hata wale wanaowatesa Wakristo, kama Paulo alivyofanya wakati fulani, wanaweza kufanya hivyo bila kusumbuliwa na dhamiri kwa sababu wanafikiri kwamba Mungu anakubali matendo yao. Ni muhimu dhamiri yetu isitusumbue kwa njia yoyote na pia iwe safi machoni pa Mungu.—Matendo 23:1; 2 Timotheo 1:3.