Maelezo ya Chini
b Kwa kawaida, zawadi za roho takatifu zilipitishwa kupitia mitume. Hata hivyo, katika hali hii isiyo ya kawaida, inaonekana Yesu alimwamuru Anania apitishe zawadi za roho takatifu kwa Sauli. Baada ya kugeuzwa imani, kwa muda fulani, Sauli alikuwa peke yake, mbali na wale mitume wengine 12. Hata hivyo, inaonekana kwamba aliendelea kuwa mtendaji katika kipindi hicho. Inaonekana kwamba Yesu alihakikisha Sauli amepata nguvu zinazohitajika ili kuutimiza mgawo wake wa kuhubiri.