Maelezo ya Chini
b Daktari mmoja ambaye pia ni mwandishi wa vitabu, aliandika kwamba huenda ugonjwa ambao Yosefo na Luka wanataja ulisababishwa na minyoo iliyoziba utumbo. Nyakati nyingine mtu mwenye ugonjwa huo hutapika minyoo au, anapokaribia kufa, minyoo hiyo hutoka. Kitabu kimoja kinasema: “Maneno hususa ya kidaktari anayotumia Luka yanafafanua vizuri kifo chenye maumivu kilichompata [Herode].”