Maelezo ya Chini
b Yakobo alirejelea kwa busara maandishi ya Musa ambayo zaidi ya kuwa na Sheria, yalitia ndani masimulizi ya jinsi Mungu alivyoshughulika na watu wake na maoni yake kabla ya Sheria kutolewa. Kwa mfano, maoni ya Mungu kuhusu damu, uzinzi, na ibada ya sanamu yanaonekana wazi katika kitabu cha Mwanzo. (Mwa. 9:3, 4; 20:2-9; 35:2, 4) Hivyo, Yehova alionyesha kanuni zinazowahusu wanadamu wote iwe ni Wayahudi au Watu wa Mataifa.