Maelezo ya Chini
e Watu fulani husema kwamba Paulo alikuwa akirejelea tukio hili alipowaambia Wakorintho “hatukuwa na uhakika hata kuhusu uhai wetu.” (2 Kor. 1:8) Hata hivyo, huenda alikuwa akizungumzia pindi nyingine iliyokuwa hatari zaidi. Paulo alipoandika kwamba ‘alipigana na wanyama wa mwituni huko Efeso,’ huenda alikuwa akizungumzia wanyama wakali katika uwanja fulani wa michezo au wanadamu wapinzani. (1 Kor. 15:32) Inawezekana alikabili hali hizo kihalisi au kwa njia ya mfano.