Maelezo ya Chini
b Miaka michache baadaye, mtume Paulo aliandika barua yake kwa Waebrania, ambamo alithibitisha ubora wa agano jipya. Katika barua hiyo, alionyesha wazi kwamba kuanzishwa kwa agano jipya kuliondolea mbali agano la kale. Mbali na kutoa hoja zenye kusadikisha ambazo Wakristo Wayahudi wangeweza kutumia kuwajibu Wayahudi waliowapinga, hoja za Paulo ziliimarisha imani ya baadhi ya Wakristo waliokuwa wakishikilia kupita kiasi Sheria ya Musa.—Ebr. 8:7-13.