Maelezo ya Chini
d Watu fulani wamesema kwamba inawezekana Paulo hakuwa akiona vizuri kwa hiyo hakumtambua kuhani mkuu. Au huenda alikuwa mbali na Yerusalemu kwa muda mrefu sana hivi kwamba hakumjua kuhani mkuu wa wakati huo. Au kwa sababu ya umati wa watu uliokuwapo labda Paulo hangeweza kuona ni nani aliyetoa amri apigwe.