Maelezo ya Chini
b Kulingana na Danieli 1:1, 2, Yehoyakimu alitiwa mkononi mwa Nebukadneza katika mwaka wa tatu wa kuwa kwake kibaraka. Huenda hilo likamaanisha kwamba mfalme huyo alikufa wakati wa mazingiwa, ambayo hatimaye yalifanikiwa. Inawezekana kwamba, kama mwanahistoria Yosefo alivyoandika, Nebukadneza alimuua Yehoyakimu na kuagiza mwili wake utupwe nje ya kuta za Yerusalemu bila kuzikwa. Hata hivyo, Biblia haisemi lolote kuhusu jambo hilo.—Yer. 22:18, 19; 36:30.