Maelezo ya Chini
a Neno la kibiolojia faila linarejelea kikundi kikubwa cha wanyama wenye sifa zinazofanana. Njia moja ambayo wanasayansi huainisha vitu vyote vilivyo hai ni kwa kutumia mfumo wa hatua saba, ambapo kila hatua iko wazi zaidi kuliko ile inayoitangulia. Hatua ya kwanza ni himaya, ambayo ndiyo kikundi kikubwa zaidi. Kisha faila, tabaka, oda, jamii, jenasi, na spishi. Kwa mfano, farasi ameainishwa kwa njia ifuatayo: himaya, Animalia; faila, Kodata; tabaka, Mamalia; oda, Perissodactyla; jamii, Equidae; jenasi, Equus; spishi, Caballus.